Lionel Messi ashinda Ballon Dor 2019


Nahodha wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentina, Lionel Messi, ameshinda tuzo ya Ballon Dor 2019 katika sherehe zilizofanyika usiku huu Jijini Paris Ufaransa.

Messi amewashinda beki wa Liverpool Virgil van Dijk aliyeshika nafasi ya pili, pamoja na Cristiano aliyekamata nafasi ya tatu huku Sadio Mane akiwa nafasi ya nne.