Wasi wasi umeongezeka kati ya Tehran na Washington tangu mwaka 2018, wakati Marekani ilipojitoa kutoka makubaliano ya kinyuklia ya mwaka 2015 kati ya Iran na mataifa sita makubwa duniani na rais Donald Trump kurejesha vikwazo dhidi ya Iran, na kuathiri mauzo muhimu yake ya mafuta.
Iran mara kadhaa imetishia kufunga ujia huo wa bahari iwapo mauzo ya mafuta yake ghafi yatazuiwa na vikwazo vya Marekani, hatua ambayo Marekani imesema itafikia kuvuka msitari mwekundu na hatua hiyo itahitaji kupatiwa jibu.