Kenya yapunguza malipo ya utalii ili kufufua sekta hiyo


Serikali ya Kenya jana imetangaza kupunguza ada za kuingia Mbuga Kuu za Wanyamapori kwa Watalii kutoka ndani na nje ya nchi ili kufufua sekta ya utalii iliyoathiriwa sana na janga la COVID19

Taarifa iliyotolewa na Shirika la Huduma za Wanyama Pori nchini Kenya (KWS) limesema hatua hiyo itadumu kwa mwaka mmoja

Pia, shirika hilo limewaruhusu wamiliki wa nyumba za kulala wageni kwenye Hifadhi za Wanyamapori wasitishe kulipa kodi kwa mwaka 1 kuanzia tarehe Mosi mwezi Julai hadi tarehe 30 mwezi Juni mwaka ujao

Waziri wa utalii, Najib Balala amewataka wamiliki hao kuboresha huduma za watalii na kukuza biashara zao kwa kutumia akiba inayotokana na usitishaji wa kodi

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia