Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt,Anna Mghwira amesema Mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro alipata wakati mgumu wa namna ya kupeleka majibu ya vipimo vya homa ya Mapafu (COVID- 19).
Dkt Mghwira ameyasema hayo wakati wa tamasha la shukrani kwa Mungu kwa kuliepusha taifa na virusi vya Corona,tamasha lililoenda sambamba na uzinduzi wa wimbo wa Dkt Mghwira kuhusu ugonjwa huo.
