https://monetag.com/?ref_id=TTIb Milk Shake Moja Ukinywa Ni Sawa Na Umeramba Sukari Kavu Vijiko 39. | Muungwana BLOG

Milk Shake Moja Ukinywa Ni Sawa Na Umeramba Sukari Kavu Vijiko 39.

SUKARI IMEFANYA VIJANA WENGI HAWANA NGUVU ZA KIUME KWA KUNYWA HOVYO
VINYWAJI VYA SUKARI ETI WANAPOZA KOO NA KUONGEZA NGUVU.

4. Sukari ndiyo Inafanya FAMILIA NZIMA MNANENEPA, Kuanzia BABA, Mama na WATOTO wote Mnakuwa NI KITAMBI. Sukari Sukari.

Tunaposema Sukari Mtambue kwamba Inakuja katika SURA TOFAUTI TOFAUTI wengi tunapumbazika kwamba ni ILE TU INAYOKUJA NYEUPE KAVU.

1. Kwenye Soda Kasome kuna Gram ngapi za sukari halafu jibu utakalopata gawanya kwa 5gram ili upate vijiko. Mfano: Ukikuta kuna gram 37 kwenye kinywaji chako Gawanya kwa 5 utapata vijiko 7 unalamba kila unywapo kinywaji hicho. Fanya Uchunguzi Ujue unalamba vijiko vingapi kwa siku.

Watu wanakunywa soda Zaidi ya 5 kwa siku.

2. Mbali na hivyo Kuna Vinywaji vingine kama MILK SHAKES, MAZIWA YA UNGA, MAZIWA YA MILK FORMULA YA WATOTO, COCKTAILS,huko Pia UTAIKUTA SUKARI.

3. Sukari Pia utaikuta kwenye JUISI TUNAZOTENGENEZA NYUMBANI SHAKES ZA MATUNDA Mfano: Unachukua Maembe mengi, Machungwa unatengeneza Juisi nzito. Utakutana na neno NO ADDED SUGAR Usipumbazwe na hilo. Unapokunywa JUISI HIO NI SUGAR SYRUP Kuna watu wanatupotosha sana.

Unapoambiwa Embe lina faida kwa afya Haimaanishi Utengeneze Juisi Unapoambiwa Nyanya, Papai lina lycopene ambayo huua kansa seli haimaanishi utengeneze juisi ya nyanya na Papai upone kansa Unapoambiwa Beet root na karoti zina faida kiafya haimaanishi utengeneze JUISI Unapoambiwa STAFELI lina ACTIVE INGREDIENTS inayotibu kansa Haimaanishi UNYWE JUISI YA STAFELI UTAPONA KANSA.

Hata hivyo Vitamin ambazo hupatikana kwenye Matunda huitwa WATER SOLUBLE VITAMINS, Ambazo ni B vitamins na Vitamin C. Kisayansi Vitamin hizi huwa Zinapozidi mwilini HUWA HAZIWEZI KUHIFADHIWA MWILINI, ZINATOKA PAMOJA NA MAJI YANAYOTOKA MWILINI. Kwa maana hio KUNYWA GLASI TANO ZA EMBE NA MACHUNGWA UTAKUWA UNAJIUMIZA KIAFYA, UNAMIMINA SUKARI NYINGI KWA MKAO MMOJA KWA LENGO AMBALO HALIENDI KUTIMIA.

Mwili wa binadamu huwa unahifadhi vitamins zinazotembea na MAFUTA ambazo ni Vitamin A,D,E na K hizi huhifadhiwa Mwilini pale unapokula nyingi. Ambapo sasa anayekunywa JUISI ILI APATE VITAMINS NYINGI ANAKULA ANAJIPUMBAZA BURE hakuna CHOCHOTE ANACHOPATA TOFAUTI NA KUUMIZA INI LAKE.

Kwa maana Hio SIKUSHAURI UTENGENEZE JUISI MATUNDA YAKO KWA WATOTO WAKO NA FAMILIA YAKO. Waliotuambia Tunatibu kwa mboga mboga za matunda walitupotosha sana TUMEHAMA KUTOKA KWENYE SODA TUMEAHAMIA KWENYE VIMIMINIKA VYA SUKARI TUNAVYO TENGENEZA SISI WENYEWE.

Athari za Sukari Mwilini.
ZINAKUHATARISHA KUPATA MAGONJWA YA UCHAKAVU WA MWILI MAPEMA SANA KATIKA UMRI WAKO.