https://monetag.com/?ref_id=TTIb Chuo kikuu kikubwa Afrika Kusini chaweka ulazima wa chanjo ya Covid-19 | Muungwana BLOG

Chuo kikuu kikubwa Afrika Kusini chaweka ulazima wa chanjo ya Covid-19


Chuo Kikuu cha Cape Town nchini Afrika Kusini kumeweka ulazima wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Covid-19 na kwamba utekelezaji wa hatua hiyo utaanza Januari.
 
 Ufafanuzi wa mpango huo utatolewa Desemba na kwamba hatua hiyo itakifanya chuo kikubwa kuwa cha kwanza kuweka masharti ya chanjo ili mtu aweze kuingia katika maeneo yake. 
 
Afrika Kusini hivi karibuni ilizindua cheti cha chanjo cha kieletroniki na kwa sasa kipo katika mjadala kama matumizi yake yawe ya lazima katika baadhi ya maeneo au la.
 
Taifa hilo ambalo limeathiriwa vibaya zaidi na virusi vya corona barani Afrika, limeanza taratibu kutoa chanjo kwa raia wake huku likikabiliana na hali ya kusitasita.

 

Post a Comment

0 Comments