Mawaziri wa ulinzi wa kutoka mataifa 30 wanachama wa Jumuiya ya Kujihami NATO wanakutana ana kwa ana kwa mara ya kwanza baada ya zaidi ya mwaka mmoja na nusu, kwenye makao makuu ya muungano huo mjini Brussels
Mada za kujadiliwa katika mkutano huo ni ujenzi zaidi wa uwezo
wa jumuiya hiyo kuzuwia hujuma na kujilinda, pamoja na juhudi
zinazoendelea za kuwarudisha nyumbani wafanyakazi wa jumuiya hiyo
waliosalia nchini Afghanistan.
Zaidi ya hayo, mkutano huo utajadili
namna ya kuendeleza mipango ya kuwekeza katika teknolojia zinazoinukia.
Kwa muktadha wa kutimiza lengo hilo, mfuko wa ubunifu wenye thamani ya
takribani Euro bilioni moja unapangwa kuanzishwa. Mkutano huo hata hivyo
umegubikwa na mzozo mpya kati ya jumuiya hiyo na Urusi.