F Takriban wafanyakazi 20 wa mgodi wafariki katika ajali ya barabarani Afrika Kusini | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Takriban wafanyakazi 20 wa mgodi wafariki katika ajali ya barabarani Afrika Kusini

 


Takriban watu 20 wamefariki dunia nchini Afrika Kusini baada ya ajali kubwa ya barabarani katika jimbo la kaskazini la Limpopo.


Waathiriwa - wanaoaminika kuwa wachimba migodi - walikuwa kwenye basi ambalo liligongana na lori


Walikuwa wakisafirishwa hadi kwenye migodi mikubwa ya almasi nchini - Venetia - inayomilikiwa na kampuni kubwa ya madini ya De Beers.


Venetia, karibu na mipaka na Botswana na Zimbabwe, inachangia zaidi ya 40% ya uzalishaji wa almasi wa kila mwaka wa Afrika Kusini.

Post a Comment

0 Comments