Netanyahu anasema kunaweza kuwa na mpango wa kuwaachilia mateka wa Israel


Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameulizwa kama kunaweza kuwa na makubaliano ya kuwakomboa mateka takriban 240 wa Israel waliotekwa wakati wa shambulio la Oktoba 7.


"Unnaweza kuwepo'', alikiambia kituo cha TV cha Marekani NBC.


"Kadiri ninavyozungumzia kidogo jkuhusu suala hili, ndivyo nitakavyoongeza uwezekano wa kutokea."


Bw Netanyahu hakutoa maelezo yoyote lakini alisema "jambo moja" ambalo linaweza kulazimisha makubaliano ni "shinikizo la kijeshi" ambalo jeshi lake la ulinzi lilikuwa likifanya dhidi ya Hamas.


Lakini afisa mmoja wa Marekani ambaye jina lake halikutajwa amedai kuwa muda wa usitishaji mapigano ni "muhimu" katika mzozo huo ili kuruhusu kkuachiliwa kwa mateka.


Waziri Mkuu Netanyahu amekataa wito unaoongezeka wa kusitishwa kwa mapigano na ameapa kuwa usitishaji huo utatekelezwa iwapo utaambatana na kuachiliwa kwa mateka wote.

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia