Oryx Gesi yagawa mitungi ya gesi ya kilo 15 na majiko yake 100 kwa wahariri na waandishi


Na Mwandishi Wetu
          
KAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi ya gesi ya kilo 15 100 yakiwa na majiko yake yenye sahani mbili kwa wahariri na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali ikiwa ni sehemu ya mpango wake wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Akizungumza leo Aprili 30,2024 wakati wa hafla fupi ya ugawaji wa mitungi hiyo  iliyofanyika Kigamboni Dar es salaam Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo Benoit Araman amesema lengo la kugawa mitungi kwa waandishi ni muendelezo wa kuunga mkono juhudi za za Rais Dk Samia Suluhu Hassan ambaye amedhamiria kuona matumizi ya nishati safi yanapewa kipaumbele.

Ameeleza kuwa Oryx imekuwa na kampeni maalum ya kuhakikisha inaiwezesha jamii kutumia nishati safi,hivyo imekuwa ikigawa mitungi bure kwa makundi mbalimbali katika jamii na leo wamewafikia Wahariri na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari.

"Tunafahamu kuwa waandishi wa habari  wanamchango mkubwa wa kuleta mabadiliko chanya, wanafanya kazi kubwa ya kuuhabarisha umma Hivyo kwa kutambua mchango wao hivyo Oryx tumeona ni busara pia kugawa mitungi kwa wadau hawa muhimu ambao wahariri na waandishi wa habari.

"Oryx Gas tukio hili tumelipa uzito mkubwa na hii inatokana na umuhimu wenu katika jamii yetu.Kwetu  vyombo vya habari vimekuwa daraja na kiunganishi kikubwa cha kufikisha taarifa zinazohusiana na nishati safi ya kupikia na hasa inayotokana na gesi ya oryx kwa jamii,"amesema Araman.


Amefafanua Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ameeleza dhamira yake kubwa  ni kuona ifikapo mwaka 2032 asilimia 80 ya Watanzania iwe inatumia nishati safi ya kupikia, Oryx Gas wamedhamiria kwa vitendo kufanikisha ndoto ya Rais

"Tumekuwa tukigawa mitungi ya gesi na majiko yake bure kwa makundi mbalimbali yakiwemo ya baba na Mama Lishe,watumishi wa sekta ya afya na wajasiriamali.Tunayofuraha leo kukutana nanyi wahariri na waandishi wa habari katika tukio hilo la kuwakabidhi mtungi wa gesi wenye kilo 15 ukiwa na plate zake mbili

Aidha amesema kama ambavyo wamekuwa wakiahidi siku zote wataendelea na kampeni hiyo kadri ya uwezo wao lengo ni kuona wanafikiwa wananchi wengi zaidi

"Oryx Ges Tanzania mpaka sasa tumeshatoa mitungi ya gesi zaidi ya 33,000 maeneo mbalimbali nchini na kiasi cha Sh  bilioni 1.5 kimeshatumika,"amesema na kuongeza wanakabidhi mitungi hiyo kwa Wahariri na waandishi wakiamini  ni kundi lenye ushawishi mkubwa hivyo watahamasisha na kuwa mabalozi kwa jamii.


 

Post a Comment

0 Comments