F JKT YATANGAZA NAFASI KWA VIJANA ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JESHI HILO KWA KIJITOLEA | Muungwana BLOG

JKT YATANGAZA NAFASI KWA VIJANA ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JESHI HILO KWA KIJITOLEA

 


Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele ametangaza nafasi kwa vijana wa Tanzania Bara na Visiwani kujiunga na mafunzo ya jeshi hilo kwa kijitolea kwa mwaka 2026 huku akionya kuwa nafasi hizo haiuzwi na Vijana, wazazi na walezi kuwaepuka matapeli watakaojitokeza kuwa wanauza nafasi hizo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema utaratibu wa vijana hao kuomba kujiunga na mafunzo hayo utaratibiwa na Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Wilaya Bara na Visiwani.

“Utaratibu wa vijana kuomba hatimaye kuchaguliwa kujiunga na mafunzo hayo unaratibiwa na ofisi za Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambako muombaji anaishi kwa vijana wa Bara na Visiwani” amesema

Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema vijana wenye taaluma za Diploma in information Technology, Diploma in Business Information System, Diploma in Computer Science, Diploma in information and Communication and Technology ICT.

Taaluma nyingine ni Diploma in Cyber security and Digital forensics, Bachelor of science in Computer science, Bachelor of Science Information Technology, Bachelor of Science in Computer Engineering, Bachelor of Science in Business Information Technology, Bachelor of Science in Cyber Security and Digital Forensics.

Wengine ni Bachelor of Science in Computer Networks and Information Security Engineering na vijana wenye vipaji vya michezo mbalimbali watapewa kipaumbele na wanashauriwa kujitokeza kwa wingi kupitia mikoa yao.

Amesema Usajili wa vijana hao kujiunga na mafunzo ya JKT kwa kujitolea utaanza tarehe 26 mwezi wa kwanza 2026 kwa mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani na vijana watakaoteuliwa watatakiwa kuripoti kwenye makambi ya JKT mwezi wa pili tarehe 27 hadi tarehe 04 mwezi wa tatu 2026.

Aidha ameendelea kusisitiza kuwa vijana watakaopata fulsa hiyo kuwa JKT halitoi ajira, pia wala halihusiki kuwatafutia ajira kwenye asasi, vyombo vya ulinzi na usalama, mashirika mbalimbali ya serikali na yasiyokuwa ya serikali bali hutoa mafunzo yatakayowasaidia vijana kujiajiri wenyewe mara baada ya kumaliza mikataba na JKT.

Amesema sifa za muombaji na maelekezo ya vifaa wanavyotakiwa kwenda navyo yanapatikana katika Tovuti ya JKT ambayo ni www.jkt.mil.tz , amesema Mkuu wa JKT anawakaribisha vijana watakaopata fursa hiyo kwenda kujiunga na vijana wenzao ili kujengewa uzalendo, umoja wa kitaifa, ukakamavu, kufundishwa stadi za kazi, stadi za maisha na utayari wa kulijenga na kulitumikia taifa lao.

Chapisha Maoni

0 Maoni