WASIFU WA MELI YA TITANIC
RMS Titanic ilikuwa meli kubwa ya abiria ya Uingereza ambayo
ilizama katika kina bahari cha Kaskazini mwa Bahari ya Atlantic mwaka 1912
tarehe 15 mwezi machi.
Meli hiyo kubwa sana ilizama wakati ilipogonga mwaba-bahari
(Iceberg)wakati ikisafirisha abiria kutoka eneo la Southampton, nchini
Uingereza ikielekea nchini Marekani katika jiji la New York.
Meli hiyo ilipozama jumla ya abiria 1,502 walipoteza maisha
katika ajali iliyorekodiwa katika vitabu vya historia vya Uingereza kama ajali
mbaya zaidi kuwahi kutokea baharini katika wakati wa amani.
Meli hiyo iliyokuwa ikimilikiwa na kampuni ya White Star
Line, wakati ikizama ilikuwa ndiyo meli kubwa zaidi duniani.
Mjenzi wa meli hiyo ilikuwa ni kampuni ya Harland and Wolff
shipyard ya Belfast.
Wakati ikizama TITANIC ilikuwa imebeba abiria jumla ya 2,224
pamoja na wafanyakazi wa meli.
Kwa mujibu wa Historia meli hiyo wakati ikizama ilikuwa
imewabeba baadhi ya matajiri wakubwa wa dunia kwa wakati huo lakini pia watu wa
kawaida kama vile wahamiaji waliokuwa wakihama Uingereza yaani Great Britain
,Ireland na Scandinavia kwenda Amerika ya Kaskazini kutafuta maisha.
Meli hiyo iliundwa kama meli kubwa ya starehe ambapo ndani
ilikuwa na mabwawa ya kuogelea maarufu kwa kiingereza kama Swimming Pool
,Maktaba,Hotel za hadhi ya juu,na Kibini za gharama kwa ajili ya abiria wenye
uwezo mkubwa sana wa kifedha.
Pamoja na kutengenezwa katika muundo wa kisasa kwa wakati
huo ambao ungewezesha kupatikana kwa msaada wakati wa ajali bado meli hiyo ya
kifahari haikuwa na meli ndogo za kutosha kukidhi mahitaji ya kuokoa watu wote
ambao wangepata ajali kama ilivyotokea.
Wakati inazama ilikuwa na meli ndogo chache ambazo
zilisaidia kuokoa maisha ya abiria 1,178 tu.
Mara baada ya kuondoka Southampton mnamo tarehe 10 Aprili
1912, Titanic ilitia nanga Cherbourg nchini Ufaransa na Queenstown (leo Cobh)
huko Ireland kabla ya kuendelea na safari.
Ajali yenyewe ilitokea mnamo tarehe 14 Aprili 1912, kiasi
cha maili 375 (sawa na km 600) Kusini mwa Newfoundland, mara baada ya meli hiyo
kugonga mwamba muda wa saa tano na dakika 40 usiku.
Mara baada ya kugonga mwamba huo sehemu ya omo ya meli
ilipasuka na hatimaye kuruhusu maji kuingia ndani katika vyumba vya chini vya
meli hiyo hali iliyosababisha meli kuanza kuelemewa na hatimaye kuanza kuzama.
Wengi wa Abiria waliosalia katika meli hiyo walikufa mara
moja kutokana na mkondo bahari wenye baridi kali na walikufa kwa hypothermia.
Abiria wengi waliokuwa katika vyumba vya meli vya daraja la
pili inaelezwa walikufa kutokana na Mabaharia kutekeleza sera ya Okoa Watoto na
Wanawake Kwanza’’.
Saa mbili baada ya meli ya Titanic kuzama Meli ya uokozi
Cunard liner RMS Carpathia iliwasili
katika eneo la ajali ambapo ilifanikiwa
kuwaokoa manusura 705.
Ajali hiyo ambayo ililalamikiwa kwa uzembe wa vyombo vya
kudhibit usalama wa baharini ilisababisha kuboreshwa kwa sheria zinazolinda
usalama wa safari za baharini huko nchini Uingereza na Marekani.
Miongoni mwa hatua hizo ni ile ya kuanzishwa kwa sheria ya
usalama baharini ya mwaka 1914 inayojulikana kama International Convention for
the Safety of Life at Sea (SOLAS), ambayo bado inatumiwa hadi hivi leo
Katika ajali hiyo wengi wa wahanga wa ajali walipoteza mali
zao zikiwemo fedha lakini wengine walipoteza ndugu na jamaa zao hususani jamaa
ya wafanyakazi wa meli hiyo wa Southampton,abiria walionusurika wengi wao
walisaidiwa na mashirika ya misaada na michango iliyotolewa na serikali.
Hata hivyo masalia ya Meli hiyo bado yamo ndani ya Bahari ya
Atlantiki hadi hivi leo kina cha Futi 12,415 (sawa na Mita 3,784).
Masalia ya Meli hiyo yaligunduliwa mwaka 1985, ambapo
wataalamu wa masuala ya historia wamekuwa wakichukua vitu mbalimbali kutoka
kwenye meli hiyo na kuviweka katika Makumbusho ya Taifa ya nchi mbalimbali
duniani zikiwemo Uingereza na Marekani.
Titanic bado inabaki kuwa Meli maarufu iliyopata kujengwa
duniani katika zama za ‘historia Mpya’ na imeandikwa katika machapisho
mbalimbali vikiwemo vitabu .