Mkuu wa wilaya, felix lyaviva :wanafunzi hewa 2548 wabainika manispaa ya temeke.

 WANAFUNZI 2548  katika shule za Sekondari na Msingi 12 wamebainika  kuwa hewa katika Manispaa ya Temeke.

Akizungumza na Wakuu wa Shule wa Sekondari, Msingi, Waratibu wa tarafa na Kata, Mkuu Wilaya ya Temeke, Felix Lyaviva amesema wanafunzi hao wamechukua fedha nyingi pamoja na kuhangikia madawati.

Lyaviva amesema kuwa walimu wakuu katika shule zilizobaki wanatakiwa kuhakiki wanafunzi katika kuweza kuondokana na wanafunzi hewa katika kuweza kupanga bajeti vizuri.

Amesema kuwa wanafunzi hewa wa kwa shule za msingi 1986 na Shule za Sekondari 859 ambao wanafunzi hao walikuwemo katika madawati na kufanya nguvu zaidi kutumika kwa wanafunzi hewa hao.

Mkuu wa Wilaya Lyaviva amesema walimu waliohusika katika kufanya hivyo watachukuliwa hatua ikiwa ni kutaka wafanyakazi kufanya kazi kwa utaratibu.

Aidha amewataka wakuu wa shule kuwa na utaratibu wa kuhakiki wanafunzi ili kuweza serikali kupanga bajeti ambayo inaenda kufanya kazi iliyokusudiwa na sio bajeti kwenda kwa wanafunzi hewa
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items