Mwasiti
Mkali wa bongo fleva kwa akina dada, mrembo Mwasiti, amegoma kunyoosha maelezo kuhusu skendo inayomkabili ya kunyanganywa gari aina ya Benz alilokuwa akilitumia, na kusema hataki kulizungumzia suala hilo.
“Hapana sijui hata unazungumzia gari gani na mimi sitakagi kuongelea personal life kwenye media sijawahi hata siku moja na sitowahi” Amesema Mwasiti ambaye amewahi kutamba na ngoma kama 'Kisa Pombe' na 'Hao' na pia ni kati ya wasanii wa kike wenye sauti nzuri na wanye uwezo mkubwa wa kuimba.
Mwasiti sasa hivi amerudi tena kwenye game ya bongo fleva na wimbo mwingine unaokwenda kwa jina la 'Kaa nao' ambapo kwa sasa amepata menejimenti au uongozi mpya ambao utakuwa unamsimamia yeye na kazi zake.
Mwasiti akiwa ndani ya studio ya EA Radio
“Kwa sasa nimepata menejimenti mpya ambayo itakuwa inasimamia kazi zangu na watu hao kuna msanii pia mkubwa sana hapa Tanzania ndiyo wanamsimamia, sasa hivi nimekaa kibiashara zaidi na wao wako tayari kunisimamia. Nimefurahi sana kwa sababu mpaka sasa hivi nimewaona kama ni watu ambao wako serious na kazi na nimependa wanavyonihandle wanataka kujua ratiba yangu ya siku nzima pia hata ukiwa studio wanakuwa na wewe na kukupa idea , wameinvest na wao ndio wanafanya kila kitu”
