Washington (CNN): Rais Barack Obama ameagiza uchunguzi ufanyike kuhusu tuhuma za udukuzi zilizofanywa na nchi ya Urusi katika kipindi cha uchaguzi mkuu wa Marekani uliofanyika Novemba 8 mwaka huu ambapo bwana Donald Trump wa Chama cha Republican aliibuka mshindi kwa kumbwaga mpinzani wake, Bi. Hillary Clinton.
