Waziri Mkuu ajiuzulu, ili kujikita na Kampeni Urafansa


Waziri Mkuu wa Ufaransa Manuel Valls amejiuzulu wadhifa wake, ili kujikita katika kampeni za kuwania urais katika uchaguzi utakaofanyika Mei mwaka ujao. Waziri wa mambo ya ndani, Bernard Cazeneuve, ameteuliwa kuwa waziri mkuu mpya.

Valls amejiuzulu siku moja baada ya kutangaza nia yake ya kugombea urais, baada ya Rais Francois Hollande kuamua kutogombea muhula wa pili kwa tiketi ya chama chao cha kisoshalisti.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items