Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI George Simbachawene amewataka wakuu wa mikoa, wilaya na mamlaka ya Serikali za mitaa kuwatafutia wamachinga maeneo rafiki ya kufanyia baishara badala ya kuwabughudhi kwa kuwaondoa katika maeneo wanayofanyia biashara.
Waziri Simbachawene ametoa agizo hilo jijini Dar es salaam mbele ya waandishi wa habari ikiwa ni agizo kutoka kwa Rais John Magufuli ambaye amesema haridhishwi na namna mamlaka husika zinavyoshughulikia suala la wamachinga ambapo amewataka kuangalia utaratibu mzuri utakaotumika kuwaondoa katika maeneo yao, na ikibidi kuwatafutia maeneo bora zaidi ya hayo.
Aidha amewataka watendaji hao kuangalia utaratibu mzuri wa kuwashirikisha wajasiriamali ili kupata ufumbuzi ulio shirikishi zaidi kwa kuanzia ni vema yakatengwa maeneo ya katikati ya miji yenye wateja wa bidhaa zinazouzwa kwa kuangalia uwezekano wa kufunga mtaa japo mmoja ili kutumikakwa kazi za kimachinga.
Kwa mujibu wa Waziri Simbachawene serikali imesikia kilio cha wafanyabiashara wadogo wanaotozwa ushuru mbalimbali kulingana na biashara zao tozo ambazo zinawadidimiza zaidi.
Waziri Simbachawene ametoa agizo hilo jijini Dar es salaam mbele ya waandishi wa habari ikiwa ni agizo kutoka kwa Rais John Magufuli ambaye amesema haridhishwi na namna mamlaka husika zinavyoshughulikia suala la wamachinga ambapo amewataka kuangalia utaratibu mzuri utakaotumika kuwaondoa katika maeneo yao, na ikibidi kuwatafutia maeneo bora zaidi ya hayo.
Aidha amewataka watendaji hao kuangalia utaratibu mzuri wa kuwashirikisha wajasiriamali ili kupata ufumbuzi ulio shirikishi zaidi kwa kuanzia ni vema yakatengwa maeneo ya katikati ya miji yenye wateja wa bidhaa zinazouzwa kwa kuangalia uwezekano wa kufunga mtaa japo mmoja ili kutumikakwa kazi za kimachinga.
Kwa mujibu wa Waziri Simbachawene serikali imesikia kilio cha wafanyabiashara wadogo wanaotozwa ushuru mbalimbali kulingana na biashara zao tozo ambazo zinawadidimiza zaidi.
