Agizo la JPM laangukia polisi

Dar es Salaam. Wizara ya Mambo ya Ndani imeanza kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kuwaondoa watumishi wasio askari kwenye Jeshi la Polisi.

Rais Magufuli alitoa agizo hilo, Julai 18 mwaka jana baada ya manaibu kamishna wa polisi 25 na makamishna wasaidizi waandamizi 35 kula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma.

Alisema uwapo wa watumishi hao raia ndani ya jeshi hilo kunachangia lichafuliwe na ni wakati mwafaka wa kuondolewa na kupangiwa kazi nyingine na utumishi.

Katika hafla hiyo, Rais Magufuli alimwagiza pia Mkuu wa Polisi Tanzania (IGP), Ernest Mangu kuorodhesha majina ya watumishi wote wasio raia ili warudishwe Utumishi.


JIUNGE NASI KATIKA
INSTAGRAM @Muungwanablog

FACEBOOK @Muungwana Blog

YOUTUBE @Muungwana Tube

BOFYA HAPA KU-INSTALLAPP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.