Watu 23 wafariki baada ya mashua iliyokuwa inasafirisha watu 247 kushika moto na kuteketea .

Mashua hiyo ilikuwa inapeleka watu kutoka kisiwa cha Tidung kutoka mji mkuu wa Jakarta .
Mkurugenzi mkuu wa shirika la kuokoa na utafiti la BASARNAS mjini Jakarta Hendra Sudirman alifahamisha kuwa abiria 194 wameokolewa na shughuli ya kutafuta na kuokoa bado inaendelea .
Abiria hao walikuwa wanaenda kisiwa cha Tidung kusherehekea mwaka mpya.