Jeshi la Polisi lawaonya wananchi wanaofanya manunuzi kwa njia ya mitandao



Msemaji wa Jeshi la Polisi, Mratibu Mwandamizi wa Polisi, Advera Bulimba.

Jeshi la polisi nchini limewataadharisha wafanyabiashara na wananchi wanaofanya manunuzi au kuuza bidhaa kwa njia za mtandao kuwa makini na matapeli wanaotumia mitandao kufanya uhalifu vikiwemo vitendo vya wizi.

Kauli hiyo imetolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Mratibu Mwandamizi wa Polisi, Advera Bulimba na kutoa tahadhari hiyo kutokana na kuwepo kwa matukio mengi ya watu kuibiwa fedha zao wakati wa kuuza au kununua bidhaa kwa kutumia mitandao.

“Watu wamekuwa wakifanya biashara kwa njia za mtandao na matokeo yake wanajikuta wanaingia kwenye kutapeliwa kwenye kuibiwa kwasababu tu ametuma pesa kwa mtu ambaye hamfahamu, amefanya biashara na mtu ambaye hamfahamu yani wamewasiliana tu kupitia mtandao,” alisema Bulimba.

“Kwamba mimi nafanya biashara mbili tatu, mimi nauza kitu fulani nitumie pesa kiasi fulani ntakutumia mzigo, tunaomba wananchi wawe makini na hili suala kwasababu tumepokea matokeo mengi ya wananchi kutapeliwa kwa njia ya mtandao”.


JIUNGE NASI KATIKA
INSTAGRAM @Muungwanablog

FACEBOOK @Muungwana Blog

YOUTUBE @Muungwana Tube

BOFYA HAPA KU-INSTALLAPP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.
Mpya zaidi Nzee zaidi