mara mdogo wake wa miaka (4)
Afisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Iringa Josephina Mwaipopo akiwa na mtoto aliyebakwa
Mashuhuda wa tukio hilo lililotokea January 16 majira ya saa 2 usiku walimweleza mwandishi wa OFM Iringa kuwa kijana huyo mara kwa mara alikuwa akimbaka mdogo wake huyo ambae baba mmoja na mama tofauti kabla ya mtoto huyo kuwaeleza majirani kuwa kakake huyo amekuwa akimkandamiza na kijiti sehemu zake za siri (Akimbaka)
Kutokana na maelezo ya mtoto huyo ndipo taarifa za raia wema hao zilipofikishwa kwa mkuu wa wilaya na OFM na kuamua kufika katika eneo la tukio na kufanikiwa kumkamata kijana huyo na baba mzazi wa watoto hao Shukuru Mkiwa kwa malezi mabaya ya watoto.
Akizungumza baada ya kukamatwa kwa kijana huyo mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela pamoja na kuwashukuru raia wema kwa kufikisha taaarifa ya kunyanyaswa kwa mtoto huyo bado alitoa wito kwa wananchi wengine ambao wanataarifa za kunyanyaswa kwa mtoto yeyote katika wilaya ya Iringa kutoa taarifa ili wahusika wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Kasesela alisema kuwa uchunguzi uliofanywa baada ya vipimo katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa umeonyesha mtoto huyo kashaondolewa usichana wake na hivyo kulazimika kulazwa kwa matibabu katika Hospitali hiyo huku akiahidi kumsaidia mtoto huyo kumsomesha .
Alisema kuwa yawezekana moja ya sababu ya mvua kuchelewa kunyesha katika mkoa wa Iringa ni pamoja na matukio ya kinyama kama haya ya ubakaji watoto na kuwa hatakubali kuona mbakaji anaendelea kuishi uraiani wilaya ya Iringa kwani tayari mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza kupitia kikao cha makati ya ushauri ya mkoa (RCC) aliagiza wabakaji wote wasakwe kwa udi na uvumba na yeye ameanza
kutekeleza agizo hilo.
Japo alisema alishangazwa na hatua ya baba mzazi wa kijana huyo kumficha mbakaji ndani na kudanganya kuwa hayupo wakati kijana wake alikuwepo ndani hivyo mzazi huyo kukamatwa pamoja na kijana wake yeye kwa kosa la kumchifa mharifu na kijana wake kwa kosa la ubakaji .
“Hiki ni kikosi kamili ambacho kitaendelea kuendesha misako mbali mbali kwa kushirikiana na oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers hivyo kwa yeyote anayejua wapi mtoto anafanyiwa vitendo vya kikatili piga simu hii mwandishi wa OFM Iringa 0754 026 299 tutakufikia ulipo na
kuchukua hatua”
Jeshi la polisi mkoa wa Iringa kupitia kwa kamanda wa polisi mkoa (RPC) Julius Mjengi limethibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo na kuwa baada ya upalelezi atafikishwa mahakamani huku likiwataka wananchi kuendelea kufichua waharifu zaidi
JIUNGE NASI
INSTA@MUUNGWANABLOG ,FB@MUUNGWANABLOG,YOUTUBE @MUUNGWANA TUBE, BOFYA HAPA KU-INSTALL APP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.