Mabomu ya machozi yazua kizaazaa

File Photo 

Morogoro. Polisi mjini Morogoro  wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Chadema baada ya kumalizika kwa mkutano wa kampeni katika Kata ya Kiwanja cha Ndege.

Kabla ya kurusha mabomu hayo saa 12:30 jioni, dereva wa gari la matangazo lililotumika katika kampeni hizo aliamriwa kuzima muziki huku wafuasi hao wakitakiwa kurudi nyumbani bila ya kufanya maandamano ambayo yanaweza kuhatarisha usalama.

Mkuu wa Polisi Wilaya ya Morogoro (OCD), Peter Nsato amesema walilazimika kurusha mabomu ya machozi baada ya wafuasi wa Chadema kuandamana katika mitaa mbalimbali ya kata hiyo hali ambayo ingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.


JIUNGE NASI 
 INSTA@MUUNGWANABLOG ,FB@MUUNGWANABLOG,YOUTUBE @MUUNGWANA TUBE, BOFYA HAPA KU-INSTALL APP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.
Mpya zaidi Nzee zaidi