Wajumbe Wa kamati inayoshughulikia mgogoro wa ardhi katika pori tengefu la Loliondo wameshindwa kutoa maamuzi ya hatma ya tatizo hilo baada ya hoja zilizowasilishwa na wataalam,wawekezaji na wananchi kuonekana kuwa zinazopingana na sheri zilizopo na pia kutokuwa na maslahi mapana kwa wañanchi na taifa kwa ujumla.
Miongoni mwa mwa hoja zilizotajwa kuleta mkanganyiko ni pamoja na kukiukwa kwa sheria zinazosimamia pori tengefu ,uwekezaji ,na matumizi bora ya ardhi na pia haki za wananchi.
Kutokana na hali hiyo mwenyekiti wa kamati hiyo iliyoundwa kutekeleza agizo la Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa Bw Mrisho Gambo amelazimika kuunda kamati nyingine ya wataalam ,wanasheria, wawekezaji na wananchi ya kushughulikia changamoto zilizojitokeza na kutoa tena mapendekezo.
Pamoja na changamoto hizo baadhi ya wajumbe wa kamati ya kutatua mgogoro huo unaofukuta kwa zaidi ya miaka 20 wamesema hatua iliyofikiwa ni nzuri hasa kutokana na ushirikishaji mkubwa wadau wanaoguswa na mgogoro huo wakiwemo wananchi ambao kwa sasa wameshirikishwa ipasavyo.