Mcheza tenisi wa Uingereza, Johanna Konta ametinga robo fainali ya mashindano ya wazi ya Australia, baada ya kumtoa Mrusi Ekaterina Makarova kwa jumla ya 6-1 6-4, huko Melbourne Park, mjini, Melbourne.
Konta mwenye umri wa miaka 25, sasa atakutana na kigogo wa tenesi Mmarekani, Serena Williams ambaye naye ameshinda 7-5 6-4 dhidi ya Barbora Strycova kutoka Jamhuri ya Czech.
Naye Mcroatia Mirjana Lucic-Baroni alimaliza kiu yake ya kusubiri kwa miaka 18 kutinga robo fainali kwa mashindano ya Gland Slam, baada ya kupata ushindi dhidi ya Mmarekani Jennifer Brady
Lucic-Baroni, mwenye umri wa miaka 34, alishinda kwa seti mbili za 6-4 6-2 na kutinga robo fainali kwa mara ya kwanza tangu atolewe na Steffi Graf kwenye mashindano ya Wimbledon mwaka 1999.
Konta mwenye umri wa miaka 25, sasa atakutana na kigogo wa tenesi Mmarekani, Serena Williams ambaye naye ameshinda 7-5 6-4 dhidi ya Barbora Strycova kutoka Jamhuri ya Czech.
Naye Mcroatia Mirjana Lucic-Baroni alimaliza kiu yake ya kusubiri kwa miaka 18 kutinga robo fainali kwa mashindano ya Gland Slam, baada ya kupata ushindi dhidi ya Mmarekani Jennifer Brady
Lucic-Baroni, mwenye umri wa miaka 34, alishinda kwa seti mbili za 6-4 6-2 na kutinga robo fainali kwa mara ya kwanza tangu atolewe na Steffi Graf kwenye mashindano ya Wimbledon mwaka 1999.
