Siku za majaribio ya Ajibu Misri zimeisha

Mshambuliaji wa Simba, Ibrahom Ajib kwa kiasi kikubwa amekonga nyoyo za mashabiki wa Haras El Hodood ya Misri baada ya kucheza mechi yake ya kwanza ya kirafiki na kufunga bao.
Awali, Haras el Hodood waliwaambia Simba jana Desemba 31, 2016 ndiyo siku ya mwisho ya majaribio. Maana yake jibu linatakiwa kutolewa leo.

Lakini kwa upande wa wachezaji wenzake wameonyesha kuvutiwa naye kutokana na namna alivyokuwa msaada katika mechi hiyo ya kirafiki waliyoshinda kwa mabao 4-0.

Katika picha mbalimbali zilizozagaa mitandaoni, Ajibu ameonyesha kuwa karibu na wachezaji wenzake licha ya kuwa mgeni.

Awali, uongozi wa Simba ulisema, Ajibu alifuzu vipimo vya afya na ilikuwa limebaki suala la benchi la ufundi kutoa uamuzi.


Haras El Hodood ambao walipomoroka hadi daraja la kwanza, inatarajiwa kutoa jibu leo au kesho kuhusiana na Ajibu.

Mpya zaidi Nzee zaidi