Uhusiano wa tanzania na china unachochea uchumi – mama samia.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 70 na laki nne kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Chato kutoka kwa Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam leo wakati hafla ya kufungua sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa Jamhuri ya watu wa China.China inasherehekea Mwaka Mpya ambapo mwaka huu umepewa jina la Jogoo (Rooster).

 Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Dkt. Lu Youqing akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam.

 Baadhi ya washiriki wa maadhimisho hayo wakifuatilia mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea katika hafla ya kuadhimisha mwaka mpya wa China leo jijini Dar es Salaam.

 Baadhi ya washiriki wa maadhimisho hayo wakitembelea baadhi ya mabanda yaliyopo katika viwanja vya Mnazi Mmoja ikiwa ni sehemu ya maadhimisho yam waka mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. China wanasherehekea mwaka mpya leo na kesho katika viwanja vya Mnazi Mmoja kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 11 jioni.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali ya Tanzania na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu Youqing baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam.Maadhimisho hayo yanafanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja kuanzia saa 4;00 asubuhi hadi saa 11 jioni na yanatarajiwa kumalizika kesho tarehe 22 Januari 2017.

JIUNGE NASI KATIKA
INSTAGRAM @Muungwanablog

FACEBOOK @Muungwana Blog

YOUTUBE @Muungwana Tube

BOFYA HAPA KU-INSTALLAPP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.
Mpya zaidi Nzee zaidi