Usichokijua kwenye remix ijayo ya Aje ya Alikiba

Aje ni wimbo wa Alikiba uliompa mafanikio makubwa mwaka jana ikiwemo tuzo kadhaa za video bora ya mwaka ikiwemo ile ya Soundcity MVP Awards.

Baada ya kuwepo version yenye verse toka kwa rapper Jude ‘M.I’ Abaga aka Mr Chairman wa Nigeria iliyovuja hata kabla ya official video, mashabiki walikuwa wamekaa tamaa kuwa hakutokuwepo na official remix yake.

Habari njema ni kuwa, Alikiba anaileta remix official ya Aje. Na tena itakuwa ni video.

“Ndio, remix inayokuja ndio ambayo yuko M.I na ina utofauti than the one that leaked,” meneja wa Alikiba, Seven ameyasema hayo. Seven amewataka mashabiki wawe tayari muda wote sababu remix hiyo itaachiwa kwa kushtukiza.

“He will just release it when it’s ready,” ameongeza. “Hatutoi official release date. It will drop unexpectedly.”

JIUNGE NASI KATIKA
INSTAGRAM @Muungwanablog

FACEBOOK @Muungwana Blog

YOUTUBE @Muungwana Tube

BOFYA HAPA KU-INSTALLAPP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.

Mpya zaidi Nzee zaidi