VIDEO: Kauli za Mbowe na Kafulila wakati wa kukabidhiwa kadi ya Mwanachama CHADEMA

Image result for kafulila chademaHuenda taarifa za David Kafulila kuhamia CHADEMA akitokea NCCR zitakuwa zimekufikia lakini hakuwa amekabidhiwa kadi yake ya kuwa Mwanachama, sasa jana jioni mbele ya mkutano mkuu wa CHADEMA Mwanza usajili ukakamilishwa.

Kabla ya kumkabidhi kadi Mbowe alisema yafuatayo >>> ‘Leo tunampokea rasmi tena Mh. David Kafulila ambaye amerudi kwenye chama alichokua amekizoea na kushiriki kukijenga, Mh. Kafulila hapo katikati alipata ajali ya kisiasa lakini tunamshukuru hakwenda CCM akaenda chama kingine cha upinzani‘

Baada ya kupewa kadi yake David Kafulila amesema >>> ‘Niwashukuru Wajumbe wote na viongozi wakiwemo Mawaziri wakuu wastaafu kwa namna ambavyo mmeendelea kukijenga chama hiki ambacho cha kweli hiki chama ndio nyumbani kwetu haswaa‘

Unaweza kutazama hii video hapa chini kujionea ilivyokua…
JIUNGE NASI 
 INSTA@MUUNGWANABLOG ,FB@MUUNGWANABLOG,YOUTUBE @MUUNGWANA TUBE, BOFYA HAPA KU-INSTALL APP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.
Mpya zaidi Nzee zaidi