Yanga, Azam dimbani leo Zanzibar

MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi 2017 inaendelea leo kwa mechi mbili za Kundi B kupigwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Image result for yanga fc
Mabingwa wa zamani wa michuano hiyo, Azam FC watacheza na Zimamoto kuanzia Saa 10:00 jioni, kabla ya mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga kumenyana na Jamhuri ya Pemba kuanzia Saa 2:30 usiku. 

Mechi hizo zinafuatia mechi za ufunguzi za Kundi A zilizoanza Ijumaa Taifa Jang’ombe ikiilaza 1-0 Jang’ombe Boys.

Yanga kumenyana na Jamhuri ya Pemba kuanzia Saa 2:30 usiku

Na jana wenyeji KVZ walianza vibaya baada ya kufungwa 2-0 na mabingwa watetezi, URA wakati vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba waliichapa 2-1 Taifa Jang'ombe.



Yanga iliyo chini ya Kocha Mkuu Mzambia, George Lwandamina imepania kufanya vizuri kwenye michuano ya mwaka huu baada ya kutokuwa na matokeo mazuri kwa miaka minne iliyopita.
Mpya zaidi Nzee zaidi