Yanga kuwakosa wakali wanne vs Ashanti FA Cup

Kikosi cha Mzambia George Lwandamina, Yanga kinatarajiwa kushuka dimbani kesho kukipiga na Ashanti United kwenye mchezo wa kombe la FA unaotakaofanyika   katika uwanja Uhuru.
IMG_0275
Yanga wanashuka dimbani wakiwa ni mabingwa watetezi wa kombe hilo baada ya kumfunga Azam 3-1 kwenye fainali ya kwanza tangu michuano hiyo iliporejeshwa tena.

Akizungumza na shaffihdauda.co.tz kocha msaidizi Juma Mwambusi amesema: “Tumejianda vizuri nia yetu ni  kushinda na tuna matumaini  na vijana wetu  watajituma kulinga na tuliyowafundisha ili kutetea kombe letu.”

“Wachezaji wote wapo kwenye  hali nzuri huku wakiwa na morali ya kushinda ili kujiweka katika mazingira mazuri katika michuano hiyo ambayo ipo  katika hatua ya tano.”

Aidha Timu hiyo itawakosa baadhi ya nyota wake  ambao ni Donald Ngoma, Obrey Chirwa, Justin Zullu, Malimi Busungu  ambaye bado ana matatizo ya kifamilia.

 JIUNGE NASI 
 INSTA@MUUNGWANABLOG ,FB@MUUNGWANABLOG,YOUTUBE @MUUNGWANA TUBE, BOFYA HAPA KU-INSTALL APP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.

Mpya zaidi Nzee zaidi