Serikali imesema watanzania wanane bado wanashikiliwa katika mahabusu za nchini Malawi kwa kuingia nchini humo kinyume na taratibu na kufanya utafiti katika sehemu yanapochimbwa madini ya Uranium kinyume na taarifa zinazosambaa kuwa walitumwa na serikali kufanya shughuli za ujasusi nchini humo.
Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa balozi Dr.Augustine Mahiga ameiambia ITV kuwa alikuwa nchini Malawi kwa mambo mbalimbali ikiwemo kufuatilia kwa kina kuhusiana na watanzania hao na kwamba amekubaliana na rais wa nchi hiyo Mhe.Peter Mutharika kuwa haki itendeke kwa watanzania hao.
Nao baadhi ya wanasheria ambao ni watetezi wa haki za binadamu wamesema wanashangaa kukamatwa kwa watanzania hao kwani wao wanaamini kuwa waliingia kihalali nchini Malawi.
VIDEO: Unaujua Uchungu wa Mke? Cheki hii ya Mau Fundi
