Pamoja na kutumbuiza, Beyonce ni mmoja ya waimbaji walioshinda Grammy mwaka huu
Hata hivyo kuna faida kubwa ambayo huja baadaye kwa washindi. Mtandao wa Forbes umewahi kuripoti kuwa wasanii wanaotumbuiza huongeza asilimia 55% ya mauzo ya tiketi kwenye show zao. Watayarishaji wa muziki nao hunufaika vile vile.
Watayarishaji wa muziki wanaposhinda tuzo za Grammy huweza kuongeza bei katika kazi wanazofanya. Watayarishaji wa muziki ambao hawajashinda tuzo za Grammy hutoza wastani wa $30,000 hadi $50,000 kwa wimbo mmoja. Wakishinda tuzo hiyo gharama ya kuanzia hupanda hadi kuwa $75,000 na watayarishaji wakubwa zaidi huweza kutoza mara mbili ya hiyo.
Kwenye tuzo za Grammy mwaka huu Adele aliibuka na ushindi mzito ukiwemo wa album ya mwaka, 25
Chance The Rapper amewashangaza wengi mwaka huu kwa kushinda tuzo za 3 za Grammy bila kuwa chini ya label yoyote na muziki wake huutoa bure mtandaoni. Thamani yake inatarajiwa kupanda kwa kiasi kikubwa baada ya ushindi huo


