VETA kanda ya Dar es Salama yatangaza operesheni ya kusaka vyuo vinavyojiendesha kinyume na sheria.

Mamlaka ya elimu  na mafunzo ya ufundi  stadi  VETA kanda ya Dar es Salama imesema kumekuwepo na ongezeko kubwa la uanzishwaji wa vyuo  vya ufundi stadi kiholela ambavyo vinatoa   huduma chini ya viwango na hivyo imetangaza operesheni maalum ya kuvisaka vyuo vyote ambavyo vinajiendesha kinyume na sheria na watavichukulia hatua za kisheria ikiwemo kuvifungia.

Akizungumza  jijini  Dar es Salaam mwenyekiti wa bodi ya  VETA kanda ya Dar es Salaam Dkt. Patricia Mwesiga  amesema kutokana na kuwepo kwa vyuo holela  matokeo yake vimekuwa vinazalisha wataalamu ambao hawaendani na hali halisi  mahitaji ya soko kwa sasa.

Naye mkurugenzi wa kanda  hiyo  Bw. Habibu Buko amesema wanachofanya sasa hivi ni kujitathimini na kuweza kuzalisha wataalamu ambao wanaweza kuendana na uchumi wa viwanda ambao ndio agenda ya sasa ya serikalini na hivyo wanajukumu kubwa mbele yao.

Wakati VETA wakiyasema hayo  umoja  wa vyuo  vya ufundi  stadi  kanda ya Dar es Salaam amesema wanachoataka kutoka VETA ni kuona mamlaka hiyo inakuwa na mfumo wake unaojitegemea ili kutoa huduma bora tofauti na ilivyo sasa kuwa  baadhi ya majukumu ya VETA yanaingiliwa ama yanaingia katika nyanya zingine.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items