Hospitali ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma inakabiliwa na upungufu wa majengo na vitanda kwenye wodi ya wajawazito ambapo wajawazito wanalala wagonjwa wanne katika kitanda kimoja.
Hayo yamebainika katika kipindi hiki ambacho wanawake wako katika heka heka ya siku ya mwanamke duniani Machi 8 ambapo Mganga Mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Mbinga Dkt Jordan Nchimbi amesema wodi ya wazazi ya hospitali hiyo ni ndogo kiasi ambacho hawawezi kuongeza vitanda na hivyo wajawazito wanalala wanne katika kitanda kimoja.
Wanawake watumishi katika Halmashauri ya mji wa Mbinga wametembelea wodi ya wajawazito katika hospitali hiyo kuona changamoto zinazowakabili wanawake na kutoa misaada mbalimbali ikiwemo mashuka ambapo pia wametoa misaada katika vituo vya watoto yatima.
Mganga huyo wa hospitali hiyo ya wilaya amewashukuru wanawake hao kwa misaada hiyo na kwamba mashuka hayo yatawasaidia wagonjwa katika wodi hiyo.
Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ...
Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..
Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..
Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

