Wanawake 7 kati ya 10 wanatumia dawa za kulevya


Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Siyanga, amesema zaidi ya asilimia 70 ya waathirika wa dawa za kulevya ni wanawake.

Kamishna Siyanga alitoa kauli hiyo Jumatatu hii, jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Umoja wa Mataifa (UN) ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya ya mwaka 2016.

“Zaidi ya asilimia 70 ya watumiaji wa dawa za kulevya ni wanawake, ndilo kundi lililoathirika zaidi, jambo hili ni kubwa si Tanzania tu, bali nchi mbalimbali duniani, tunahitaji ushirikiano kuhakikisha tunalimaliza.”

Aidha Kamishna huyu alisema pamoja na mambo mengine zipo njia tatu ambazo zinapaswa kufuatwa kuhakikisha vita dhidi ya dawa za kulevya inakomeshwa nchini ambazo ni pamoja na kuzuia uingizaji, kutoa elimu na matibabu kwa waathirika huku akisisitiza kuwa hawatachukulia hatua za sheria waathiriwa wa dawa za kulevya, badala yake watawasaidia kuwapatia tiba waweze kurejea katika hali yao ya kawaida huku wakiwahoji wanakopata dawa hizo.




Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ... 

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items