Serikali imetoa onyo kwa wawekezaji wanaokiuka sheria za ajira na zile za utunzaji wa mazingira ambapo imeahidi kuanza kuwachukulia hatua kali na zakisheria ikiwa ni pamoja na kufunga viwanda vyote vitakavyobainika kukiuka sheria hizo.
Wakati serikali ya Tanzania ikipambana kutafuta wawekezaji wenye tija kwa taifa kuja kuwekeza nchini na kuongeza ajira kwa vijana wa kitanzania, kiwanda cha king dao kinachomilikiwa na raia wa kichina kinazalisha maji huku kikikiuka sheria za kazi kwa kuwalipa wafanyakazi wake shilingi 6000 kwa kutwa.
Katika kiwanda hiki maafisa wa serikali wamebaini mapungu lukuki ya kiwemo ya wafanyakazi kutokuwa na mikataba, ukiukwaji wa sheria ya mazingira ya mwaka 2004, ambapo licha ya kukifunga kiwanda hicho pia maafisa waserikali wakatangaza kukipiga faini ya shilingi milioni 20.
Kwa upandewake naibu waziri wa kazi vijana na ajira ambaye ndiye aliyeongoza oparesheni hiyo ya kushitukiza katika kiwanda hicho cha king dao, amesema hatasita kufunga viwanda vyote vitakavyobainika kukiuka sheria za kazi hasa kwa kushindwakuwapatia mikataba wakazi wake.
Wakati serikali ya Tanzania ikipambana kutafuta wawekezaji wenye tija kwa taifa kuja kuwekeza nchini na kuongeza ajira kwa vijana wa kitanzania, kiwanda cha king dao kinachomilikiwa na raia wa kichina kinazalisha maji huku kikikiuka sheria za kazi kwa kuwalipa wafanyakazi wake shilingi 6000 kwa kutwa.
Katika kiwanda hiki maafisa wa serikali wamebaini mapungu lukuki ya kiwemo ya wafanyakazi kutokuwa na mikataba, ukiukwaji wa sheria ya mazingira ya mwaka 2004, ambapo licha ya kukifunga kiwanda hicho pia maafisa waserikali wakatangaza kukipiga faini ya shilingi milioni 20.
Kwa upandewake naibu waziri wa kazi vijana na ajira ambaye ndiye aliyeongoza oparesheni hiyo ya kushitukiza katika kiwanda hicho cha king dao, amesema hatasita kufunga viwanda vyote vitakavyobainika kukiuka sheria za kazi hasa kwa kushindwakuwapatia mikataba wakazi wake.
