Rais Mstaafu wa awamu wa nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amesema ameshuhudia kiapo cha Mke wake, Mama Salma Kikwete baada ya kuteuliwa hivi karibuni kuwa mbunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Leo asubuhi nimeshuhudia kiapo cha Mke wangu Mhe. Salma Rashid Kikwete kuwa Mbunge wa Kuteuliwa Bungeni Dodoma.Ni zamu yangu kumuunga mkono,” ameandika Dkt Kikwete kupitia akaunti yake ya Twitter.
Dkt Kikwete aliingia ndani ya bunge akishangiliwa na idadi kubwa ya wabunge wa bunge hilo.
