Uingereza na Ethiopia zakubali kushirikiana katika kumaliza biashara haramu ya binadamu

Serikali ya Uingereza siku ya Ijumaa ilitangaza kufanya ushirikiano na Ethiopia katika kuangamiza biashara  haramu ya binadamu .

Kwa mujibu wa taarifa hiyo kutoka kwa ubalozi wa Uingereza jijini Addis Ababa ni kwamba mafunzo maalum yaatatolewa kwa maafisa wa ofisi za uhamiaji nchini Ethiopia ili waweze kukabiliana na biashara  hiyo haramu .

Maafisa hao watapewa mafunzo yatakayowaezesha kutambua vibali vya usafiri na viza bandia .

Mwaka jana ubalozi wa Uingereza Ethiopia na shirika la ndege la Ethiopia Airlines walishirikiana na kuweza kuzuia kesi 160 za kupanga usafiri kinyume na sheria .
Mpya zaidi Nzee zaidi