Paulinho aanza kufungua ukurasa wa magoli, Barcelona yaipiga Getafe 2-1

Paulinho akishangilia baada ya kuifungia Barcelona bao la ushindi dakika ya 84 ikiwalaza wenyeji, Getafe 2-1 Uwanja wa Coliseum Alfonso Perez katika mchezo wa La Liga. Gaku Shibasaki alianza kuwafungia wenyeji dakika ya 39 kabla ya Denis Suarez kuisawazishia Barca dakika ya 62.
Mpya zaidi Nzee zaidi