MTU mmoja huko mwenye umri wa miaka 39 huko Chhattisgarh, India, amemtoa kafara mwanaye mdogo katika kitendo cha ushirikiana kwa kumkata uume na sehemu za kichwa kwa shoka hadi kusababisha kifo chake, kwa madai ya kufukuza mapepo mabaya ‘mashetani’.
Watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi.
Polisi walisema mwili wa mtoto huyo mwenye umri wa miaka 13 ulikutwa ukiwa katika dimbwi la damu ambapo baada ya polisi kufanya uchunguzi, Patel alikiri kumwua mwanaye huyo ili kuondoa mapepo mabaya na hivyo wamemfungulia mashitaka.

