Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza "enzi mpya kwa Marekani" alipokuwa akitoa hotuba ya kitaifa kuhusu hali ya nchi Jumanne usiku.
Katika hotuba hiyo iliyotolewa kwa Bunge la Congress, aliwaambia wabunge kuwa: "Hapajawahi kutokea wakati mzuri wa kuanza kuishi ndoto za Marekani kama kipindi hiki."
Kiongozi huyo wa chama cha Republican amesema kuwa "yuko tayari kushirikiana" na Democrats kuweka kando mgawanyiko mkali wa kisiasa baina ya vyama hivyo.
Uchumi wa Marekani unakua kwa kasi, lakini umaarufu wa Bwana Trump umeendelea kushuka.
Katika hotuba yake iliyokuwa na kauli kali tofauti na wakati wa kuapishwa alipoonekana mwenye ghadhabu na kueleza "Marekani ilivyoharibiwa " mwaka mmoja tu uliopita , Bwana Trump amesema kuwa utawala wake "unajenga Marekani iliyo salama, thabiti na ya kujivunia ".
Democrat wamjibu Trump
Mjumbe wa Congress wa jimbo la Massachusetts Joseph Kennedy III, mpwa wa rais wa zamani wa Marekani John K Kennedy, atatoa mkakati wa Democrats wa kukabiliana na hotuba ya Bwana Trump.
Atajaribu kuiharibu hotuba ya Bwana Trump kwa kutaka kuongea kwa niaba ya: ''Wamarekani wanaohisi wamesahaulika na kutelekezwa".
Akielezea kusikitishwa kwake na " nchi iliyogawanyika" na kuuelezea urais wa Bwana Trump kama "fujo", Bwana Kennedy mwenye umri wa miaka 37, atasema: " katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita wengi wameishi maisha ya wasiwasi, hasira na uoga."
"Lakini hata wakati mmoja katika historia ya Marekani yetu hawataweza kuvunja uthabiti na moyo wa watu walioungana katika kulinda hali yao ya baadae."
Nyuso za hasira
Katika wakati mmoja , wajumbe wa chama cha Democratic weusi walikaa kimya kwa nyuso za hasira wakati wabunge wengine waliposimama kushangilia hotuba wakati Bwana Trump aliposema kuwa viwango vya Wamarekani weusi wasio na ajira vimeshuka kwa kiwango ambacho hakijawahi kurekodiwa .
Takriban wabunge kumi na wawili wa Democratic wanatarajiwa kupinga hotuba ya Bwana Trump katika kile ambacho kinaweza kuwa moja ya ususiaji mkubwa wa hotuba ya rais kwa taifa
Mmoja wao ni Mbunge wa Baraza la Congress jimbo la California Bi Maxine Waters, ambaye alikiambia kituo cha televisheni cha MSNBC: " Kwa nini nichukue muda wangu kwenda na kukaa kumsikiliza muongo?."
Katika hotuba hiyo iliyotolewa kwa Bunge la Congress, aliwaambia wabunge kuwa: "Hapajawahi kutokea wakati mzuri wa kuanza kuishi ndoto za Marekani kama kipindi hiki."
Kiongozi huyo wa chama cha Republican amesema kuwa "yuko tayari kushirikiana" na Democrats kuweka kando mgawanyiko mkali wa kisiasa baina ya vyama hivyo.
Uchumi wa Marekani unakua kwa kasi, lakini umaarufu wa Bwana Trump umeendelea kushuka.
Katika hotuba yake iliyokuwa na kauli kali tofauti na wakati wa kuapishwa alipoonekana mwenye ghadhabu na kueleza "Marekani ilivyoharibiwa " mwaka mmoja tu uliopita , Bwana Trump amesema kuwa utawala wake "unajenga Marekani iliyo salama, thabiti na ya kujivunia ".
Democrat wamjibu Trump
Mjumbe wa Congress wa jimbo la Massachusetts Joseph Kennedy III, mpwa wa rais wa zamani wa Marekani John K Kennedy, atatoa mkakati wa Democrats wa kukabiliana na hotuba ya Bwana Trump.
Atajaribu kuiharibu hotuba ya Bwana Trump kwa kutaka kuongea kwa niaba ya: ''Wamarekani wanaohisi wamesahaulika na kutelekezwa".
Akielezea kusikitishwa kwake na " nchi iliyogawanyika" na kuuelezea urais wa Bwana Trump kama "fujo", Bwana Kennedy mwenye umri wa miaka 37, atasema: " katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita wengi wameishi maisha ya wasiwasi, hasira na uoga."
"Lakini hata wakati mmoja katika historia ya Marekani yetu hawataweza kuvunja uthabiti na moyo wa watu walioungana katika kulinda hali yao ya baadae."
Nyuso za hasira
Katika wakati mmoja , wajumbe wa chama cha Democratic weusi walikaa kimya kwa nyuso za hasira wakati wabunge wengine waliposimama kushangilia hotuba wakati Bwana Trump aliposema kuwa viwango vya Wamarekani weusi wasio na ajira vimeshuka kwa kiwango ambacho hakijawahi kurekodiwa .
Takriban wabunge kumi na wawili wa Democratic wanatarajiwa kupinga hotuba ya Bwana Trump katika kile ambacho kinaweza kuwa moja ya ususiaji mkubwa wa hotuba ya rais kwa taifa
Mmoja wao ni Mbunge wa Baraza la Congress jimbo la California Bi Maxine Waters, ambaye alikiambia kituo cha televisheni cha MSNBC: " Kwa nini nichukue muda wangu kwenda na kukaa kumsikiliza muongo?."
