Mgombea wa Cuf asema yeye ni mzawa wa Kinondoni

Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CUF Rajabu Juma amejigamba kwamba yeye ni mzawa halisi wa Kinondoni kwa sababu amezaliwa  Mwananyamala Hospitalini.

Amesema kwamba kwa sababu yeye ni mzawa wa eneo hilo anazijua fika changamoto za jimbo lake hivyo anawaomba wapiga kura wasiache kumchagua.

“Mimi ni mzawa wa hapa nimezaliwa hapo Mwananyamala Hospitali naombeni kura zenu msiache kunichagua jamani nitahakikisha  nazitatua  changamoto za hapa’’ amesema  na kuongeza

‘’Leo nimeja hapa kuzungumza na nyinyi kujua  shida zenu, nipeni kura tarehe 17 niwe mbunge wenu’’.

‘’Leo hii uchaguzi unarudiwa na kutumia pesa nyingi za maendeleo kwa sababu ya mbunge aliyekuwepo , leo anarudi tena kuomba kura, huyu hafai’’ amesema

Mwananchi:
Mpya zaidi Nzee zaidi