Spurs yaishindilia Arsenal 1-0

Klabu ya Tottenham imefanikiwa kuchomoza na ushindi wa bao 1 – 0 dhidi ya Arsenal mchezo wa ligi kuu ya Uingereza uliyopigwa katika dimba la Wembley.

Bao pekee la Spurs limefungwa na mshambuliaji wao hatari, Harry Kane kunako kipindi cha pili baada ya dakika 45 za awali kutoka sare ya bila kufungana.

Vikosi kamili vilivyo ingia uwanjani kwa upande wa Spurs ni Lloris (7), Trippier (7), Sanchez (8), Vertonghen (8), Davies (7), Dier (7), Dembele (7), Son (7), Eriksen (7), Alli (7), Kane (8).

Waliyokuwa benchi: Wanyama (5), Lamela (6).

Wakati kwa upande wa Arsenal: Cech (6), Bellerin (7), Mustafi (7), Koscielny (5), Monreal (6), Elneny (5), Xhaka (6), Wilshere (5), Ozil (6), Mkhitaryan (5), Aubameyang (5).

Benchi kulikuwa na  Iwobi (5), Welbeck (5), Lacazette (5).

Mchezaji bora wa mchezo huo ni: Harry Kane
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items