Raia wa Syria waanza kurudi makwao

Zaidi ya raia 160,000 wa Syria wameanza kurudi katika miji yao kutoka nchini Uturuki.

Hiyo ni baada ya operesheni ambazo zimekuwa zikifanywa na jeshi la Uturuki dhidi ya magaidi katika maeneo  mbalimbali Syria.

Ripoti zinaonyesha kuwa kwa sasa ni raia 3,567,000 wa Syria wanaishi nchini Uturuki.

Operesheni ya tawi la mzaituni iliazishwa na jeshi la Uturuki mnamo mwezi Jnauari kupigana na magaidi katka mipaka yake na vilevile kuwalinda raia wa Syria.

Wizara ya  mambo ya ndani ya Uturuki imeichukulia hatua hiyo kama hatua muhimu katika kurusidha amani nchini Syria.

Wizara ya mambo ya ndani imesema kuwa wakimbizi kutoka Syria wamekuwa wakihudumiwa kama raia wa Uturuki bila tofauti yoyote.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia