'Elimu Bure yakwamisha walinzi kulipwa mishahara kwa miezi 10'



Na Ahmad Mmow, Lindi

Baadhi  walinzi wa shule  za msingi za manispaa ya Lindi  wameuomba uongozi wa manispaa hiyo uwalipe mishahara yao ya  miez kumi. Walinzi hao walitoa malalamiko na ombi hilo jana  walipozungumza na Muungwana ofisini kwao.

Mwenyekiti wa walinzi hao, Salumu Abdallah amesema halmashauri ya manispaa Lindi  mwaka 2010 iliajiri walinzi 31 wa shule za msingi  kwa mikataba ya  muda mrefu, hata hivyo tangu muda huo ulipaji wa mishahara hauridhishi.

Alisema jumla ya Tsh. Million 17 zinazotokana na mishahara ya miezi kumi hazijalipwa hadi sasa hali inayosababisha waendelee kuisha katika hali ngumu kiuchumi.

Akijibu malalamiko na ombi la walinzi hao kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Ofisa Elimu wa shule za msingi manispaa ya Lindi, Huseni kitingi alikiri kuwepo kwa deni la walinzi hao, Hali inayotokana na kuwepo sheria ya elimu bure inayozuia wazazi na walezi kuchangia elimu.


Mpya zaidi Nzee zaidi