RC Ayoub aridhishwa na kiwango cha ufaulu kidato cha nne


Na.Thabit Madai, Zanzibar.

Serikali ya Mkoa wa mjini Magharibi Unguja imesema imeridhishwa na ongezeko la kiwango cha ufaulu wa kidato cha nne kwa kipindi cha mwaka 2018 ikilinganishwa na mwaka 2017.

Imesema katika kipindi cha mwaka 2018 ongezeko hilo imefikia asilimia 70.43 ikilinganishwa na mwaka 2017 ambapo ilikuwa  asilimia 55.88.

Akizungumza leo  na waandishi wa habari ofisini kwake vuga,  Mjini Unguja  Mkuu wa Mkoa huo,Ayoub Mohammed Mahmoud alisema ongezeko hilo ni  sawa na asilimia 14.55 na kwamba hatua hiyo inatokana na  juhudi zilizofanywa na uongozi wa serikali ya mkoa huo.

Mkuu huyo aliongeza kuwa katika ongezeko la ufaulu huo umefanikiwa kuziondoa skuli  mbili za sekondari zilizokuwa katika shule 10  za mwisho zilizofanya vibaya na kwamba hatua hiyo ni matokeo chanya.

"Tumefanikiwa kuziondoa skuli  mbili za sekondari ya Langoni na Mwenge  ambazo mwaka 2017 zilikuwa katika skuli 10 za mwisho kitaifa hiyo ni moja  ya mafainikio makubwa yaliyopatikana katika mwaka 2018" alieleza

Aidha alieleza kuwa mafaniko hayo yanatokana juhudi mbali mbali zilizofanywa  na wadau wa sekta ya elimu  pamoja na Serikali ya mapinduzi ya zanzibar katika kuondoa michango  ya skuli ambapo ilikuwa na lengo  la kupunguza ghsrama na kuongeza kiwango cha elimu zanzibar.

Hata hivyo Mkuu huyo alisema idadi ya wanafunzi  waliopata ufaulu wa daraja la kwanza 147 na daraja la pili 638 na daraja la 3, 1341 na daraja la 4, 4317.

alisema katika kipindi hicho alifanikiwa  kupunguza idadi ya wanafunzi waliopata ziro na  wamefanikiwa kuongeza idadi ya wanafunzi wanaendelea na  masomo ya kidato cha tano na sita zaidi ya elfu moja.

Aidha alisema serikali ndani ya mkoa wa Mjini Magharib utatoa  zawadi ya Tablet ambazo zitakuwa na vitabu vya masomo kwa kidato cha Tano na sita  kwa wanafunzi waliopata daraja la kwanza jumla yao 147.

Hata hivyo alisema kwa upande wa walimu walifaulisha wanafunzi hao watapewa zawadi ya kiasi cha milion 30 kwa ujumla wao.
Mpya zaidi Nzee zaidi