Mifuko 148 ya sukari yakamatwa Tanga na kutaifishwa


Shehena ya mifuko ya sukari zaidi ya 148 iliyoingizwa nchini kinyume cha sheria imekamatwa mkoani Tanga na kutaifishwa.

Kamanda wa Ulinzi na Usalama Wilayani Pangani kwa kushirikiana na maafisa wa Mamlaka wa Mapato Tanzania (TRA) ndipo wamefanikisha kukamatwa kwa sukari hiyo kutokea nchini India.

Shehena hiyo imekamatwa katika Bandari Bubu ya kipumbwi iliyopo Pangani wakati ikiwa katika harakati za kusafirishwa kwenda makao makuu ya Wilaya kisha Tanga Mjini.