Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako leo ametembelea na kukagua hatua ya ujenzi wa ofisi mpya za Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia zinazojengwa kwenye Mji wa serikali Ihumwa, mkoani Dodoma na kusema kuwa ameridhishwa na hatua ya ujenzi iliyofikiwa.