Ruge Mutahaba kuzikwa nyumbani kwao Bukoba


Familia imeamua kwamba Ruge Mutahaba atakwenda kuzikwa nyumbani kwao huko Bukoba siku ya Jumatatu, siku ya Jumapili mwili utasafirishwa kwenda Bukoba.

Afya ya Ruge Mutahaba ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group (CMG) ilianza kutetereka katikati mwa 2018, na Juni mwaka huo alikwenda India kwa ajili ya matibabu na alirejea nchini Agosti 21, 2018.

Baada ya muda kidogo hakuonekana, Oktoba 2018 alipelekwa Afrika Kusini kwa matibabu, amekaa huko hadi alipofariki.

Ruge Mutahaba amefariki siku ya jana nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu ya figo. Ruge alizaliwa mwaka 1970, Brooklyn nchini Marekani, atakumbukwa zaidi kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya muziki nchini.

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia