Rais Kagame ateuliwa kuwa mwenyekiti mpya EAC

Rais wa Rwanda, Paul Kagame ameteuliwa kuwa mwenyekiti mpya pokea wa jumuiya ya Afrika mashariki katika mkutano uliofanyika hii leo mjini Arusha Tanzania.

Waliowasili Arusha ni mwenyeji Rais John Magufuli, Paul Kagame wa Rwanda, Yoweri Museveni wa Uganda na Uhuru Kenyatta wa Kenya.

 Marais wa Burundi na Sudani Kusini wametuma wawakilishi wao kwenye mkutano huo.

Viongozi hao wamekuwa katika mkutano wa faragha tangu mchana.
Mpya zaidi Nzee zaidi